Habari
Katibu Mkuu Kiongozi akutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Hifadhi ya Wakimbizi Duniani Bi. Joyce Mends-Cole - 22 Februari, 2016.
Katibu
Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, leo tarehe 22 Februari, 2016 amekutana
na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Hifadhi ya Wakimbizi Duniani (UNHCR), Bi.
Joyce Mends-Cole ofisini kwake Ikulu Dar
es Salaam.
Bi
Mends-Cole alikutana na Balozi Sefue kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza
muda wake wa kazi hapa nchini.
Katika
mazungumzo yao, Bi Mends-Cole ameishukuru Serikali ya Tanzania na Watanzania
kwa ujumla kwa ushirikiano mzuri aliopewa katika kutekeleza majukumu yake yaliyohusika
na masuala ya wakimbizi sehemu mbalimbali nchini Tanzania. Aidha ameishukuru
Serikali ya Tanzania kwa uamuzi wake wa miaka mingi na hatua inayoendelea
kuchukua kuhifadhi wakimbizi toka nchi jirani na hata kufikia hatua ya kuwapa
baadhi ya wakimbizi hao uraia.
Kwa
upande wake, Balozi Sefue alimpongeza Bi Joyce Mends-Cole kwa mafanikio
aliyopata wakati wa kutekeleza majukumu yake hapa nchini na kueleza matarajio
ya Serikali ya Tanzania ya UNHCR na wadau wengine wa kimataifa kuzipatia
ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazowakabili wakimbizi na madhara mbalimbali
yanayotokana na uhifadhi wa wakimbizi.
Mwisho alimtakia Bi Mends-Cole kila la kheri na maisha marefu ndani na nje ya utumishi wa shirika hilo la Umoja wa Mataifa.