Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi

Wasifu

Ndg. Tomothy Apiyo
Ndg. Tomothy Apiyo
Ndugu Timoth Apiyo alitumikia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia miaka ya 1960. Mara baada ya kuhitimu shahada yake katika masuala ya kilimo alifanya kazi katika Kituo cha Kilimo cha Ukiliguru. Mnamo mwaka 1960 alihamishiwa Wilayani Muheza mkoani Tanga kuwa Afisa Mifugo wa Wilaya na baadae alipata uhamisho kwenda mkoani Morogoro na kuwa Afisa Kilimo Mkuu katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo, Ilonga. Kati ya mwaka 1964 -1965 Ndugu Apiyo alifanya kazi katika Wizara ya Kilimo na baadaye alihamishiwa mkoa wa Shinyanga kuwa Afisa Mifugo. Kazi nyingine; Katika uhai wake amewahi kuwa Mkurugenzi wa Mipango katika Wizara ya Kilimo (1968) Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo Vijijini (1969) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara. Mwaka 1974 aliteuliwa na Rais Julius K. Nyerere kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.