Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi

Wasifu

Ndg. Philemon L Luhanjo
Ndg. Philemon L Luhanjo
.

Elimu

Mwaka 1977, Bw. Luhanjo alitunukiwa Diploma ya Utawala kutoka Taasisi ya Usimamizi wa Maendeleo Mzumbe (sasa Chuo Kikuu cha Mzumbe).
Alipata Shahada ya Uzamili katika masuala ya Utawala wa Umma na kubobea katika masuala ya Uchambuzi wa Sera za umma kutoka Chuo Kikuu cha Southern California mjini Los Angeles, California, Marekani (1981 - 1982).

Historia Kwa Ufupi

Ndugu Phillip L. Luhanjo, ameitumikia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu mwaka 1975 katika nyadhifa mbalimbali. Kati ya Aprili 1975 hadi Juni 1976, Ndugu Luhanjo alikuwa Afisa Tawala katika Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa na katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mijini. Kati ya Aprili 1977 hadi Juni 1983, Ndugu Luhanjo alikuwa Afisa Mipango, Uratibu wa Nguvu Kazi katika mikoa 20 ya Tanzania Bara, katika Idara ya Tawala za Mikoa. Kaimu Kamishna Msaidizi wa Mipango ya Nguvu Kazi na Mafunzo (Julai - Disemba 1983). Aliteuliwa kuwa Katibu Masaidizi wa Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu kwa Baraza la Mawaziri katika Ofisi ya Rais, Ikulu, kuanzia Januari, 1984 hadi Machi 1986. Kati ya Aprili 1986 hadi Disemba 2005, alifanya kazi kama Karani wa Baraza la Mawaziri katika Ofisi ya Rais, Ikulu.